Mtangazaji wa TV Piers Morgan ameacha kazi
katika shirika la habari la Marekani la CNN, licha ya kupewa nafasi ya
kuongeza mkataba wake.
Morgan ame tweet akisema anakwenda "kujaribu mambo mengine mapya" baada ya wakuu wa kituo hicho kumtaka asalie kwa miaka miwili zaidi. Mkataba mpya ungempa nafasi ya kuwa na mahojiano maalum ya vipindi 40.
Piers Morgan alimrithi Larry King, katika kipindi cha mahojiano, lakini kipindi hicho kilifutwa mwezi Machi kufuatia kupoteza umaarufu.
Kipindi kilianzishwa Januari 2011 kikiwa na watazamaji karibu milioni moja, lakini idadi hiyo ilipungua hadi kufikia 270,000.
"Nimekuwa na wakati mzuri katika kipindi cha miaka minne nikiwa na CNN, na nina mheshimu sana Jeff [Zuckerberg, mkuu wa CNN] pamoja na watu wote wanaofanya kazi hapo." Amesema Morgan.
Morgan ame tweet akisema anakwenda "kujaribu mambo mengine mapya" baada ya wakuu wa kituo hicho kumtaka asalie kwa miaka miwili zaidi. Mkataba mpya ungempa nafasi ya kuwa na mahojiano maalum ya vipindi 40.
Piers Morgan alimrithi Larry King, katika kipindi cha mahojiano, lakini kipindi hicho kilifutwa mwezi Machi kufuatia kupoteza umaarufu.
Kipindi kilianzishwa Januari 2011 kikiwa na watazamaji karibu milioni moja, lakini idadi hiyo ilipungua hadi kufikia 270,000.
"Nimekuwa na wakati mzuri katika kipindi cha miaka minne nikiwa na CNN, na nina mheshimu sana Jeff [Zuckerberg, mkuu wa CNN] pamoja na watu wote wanaofanya kazi hapo." Amesema Morgan.
No comments:
Post a Comment