welcome

Your welcome to Leyla Nyenzi Blog, Dodoma-Tanzania, for the only latest Audio's,Video's,Photo's, Events and Advertisement.

Monday, 26 January 2015

ALI KIBA AKANA KUJIHUSISHA NA IMANI ZA KISHIRIKINA LEADERS

ALI KIBA FOR REAL
Tamasha lililofanyika Jumamosi iliyopita pande za Leaders limezua utata baada ya vituko vingi kutokea huku staa wa Bongo Fleva,Ali Kiba kuhusishwa na imani za kishirikina baada ya kushindwa kupita getini na kuruka ukuta.

Mlinzi wa getini hapo amezungumza na Uheard na Soudy Brown alisema kuwa Ali Kiba alifika getini lakini cha kushangaza hakupita mlangoni aliruka ukuta na kuingia ndani.

‘’Ali Kiba alifika hapa wenzake mimi nilikuwa hapa getini lakini nikashangaa ameruka ukuta’,alisema mlinzi huyo.

Hata hivyo haikuishia hapo habari zinasema kuwa Ali Kiba alishindwa kumpa mkono msanii mwenzake Mwana Fa huku baunsa wake akimzuia msanii huyo kumsalimia Ali Kiba.

Katika tamasha hilo mashabiki wa mastaa wawili Ali Kiba na Diamond Platinumz walifanya vurugu kwa kurusha chupa za maji baada ya wasanii hao walivyokuwa wakipanda jukwaani kupafomu.

Hata hivyo Ali Kiba akizungumzia tukio hilo alisema halikuwa tukio la kishirikina ila alishindwa kupita getini kwa sababu watu walikuwa wengi.

No comments:

Post a Comment

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia mkito.com!

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia  mkito.com !  Bila shaka utakuwa umeusikia huu wimbo kw...