welcome

Your welcome to Leyla Nyenzi Blog, Dodoma-Tanzania, for the only latest Audio's,Video's,Photo's, Events and Advertisement.

Tuesday, 26 August 2014

POOLEY ATAJWA KUWA SHUJAA WA EBORA

William Pooley anayetibiwa mjini London, baada ya kupata maambukizo ya Ebola, anatunzwa vizuri
Familia ya muuguzi huyo wa kujitolea, aliyesafirishwa mjini London, baada ya kuambukizwa ugonjwa wa Ebola nchini Sierra Leone, wamesema amekuwa akipata matunzo yaliyo bora
Willliam Pooley mwenye umri wa miaka 29 alirudi nchini Uingereza siku ya Jumapili na amewekwa kwenye kitengo maalumu katika hospitali ya Royal Free
Bwana Pooley ambaye alikuwa amejitolea kuwahudumia wagonjwa wa mlipuko wa Ebola barani Afrika ambao umeuwa watu 1,500 ametajwa kama shujaa na taasisi moja ya hisani inayojulikana kama Shepherd Hospice aliyoifanyia kazi nchini Sierra Leone kwa vile alijua hatari zilizokuwepo lakini akaamua kusaidia
Bwana Pooley anayetoka karibu na mji wa Woodbridge, katika kaunti ya Suffolk ni Mwingireza wa kwanza kupatikana na virusi vya Ebola katika mlipuko wa ugonjwa huo uliotokea hivi karibuni. 
SWALI: KWANINI WAAFRIKA WAFE,  MZUNGU MMOJA APONE?

No comments:

Post a Comment

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia mkito.com!

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia  mkito.com !  Bila shaka utakuwa umeusikia huu wimbo kw...