welcome

Your welcome to Leyla Nyenzi Blog, Dodoma-Tanzania, for the only latest Audio's,Video's,Photo's, Events and Advertisement.

Sunday, 21 September 2014

Yanga ukuta, Azam, Simba ushambuliaji


Dar es Salaam. Pazia la Ligi Kuu Bara limefunguliwa rasmi jana, lakini ni timu tatu zinapewa nafasi kubwa ya kuwa mabingwa wa ligi hiyo msimu ujao, ambazo ni bingwa mtetezi  Azam FC, Yanga na Simba.
Licha ya timu zote hizo kuwa na nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa, Yanga  imeonekana kuwa imara zaidi katika eneo la ulinzi, wakati Azam ikiwa balaa katika kuzifumania nyavu kuliko wenzake, huku Simba ikiwa haieleweki.
Safu ya ulinzi ya Yanga inaonekana kutopitika kirahisi na hivyo washambuliaji wa timu pinzani kwenye ligi wanatakiwa kuwa na akili za ziada kuipenya ngome hiyo inayoongozwa na Kipa Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani.
Ngome ya Yanga haijaruhusu bao katika  mechi tano ilizocheza chini ya kocha mpya, Marcio Maximo, mechi nne zikiwa za kirafiki na moja ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam.
Mabingwa hao wa zamani wana washambuliaji, wanane ambao  ni Genlison Santos ‘Jaja’, Andrey Coutinho, Mrisho Ngassa, Simon Msuva, Jerry Tegete, Said Bahanuzi, Hussein Javu na  Hamis Kiiza.
Azam yenyewe imeonekana kuwa hatari zaidi upande wa kuzifumania nyavu  kwani katika mechi  12 ilizocheza zikiwamo za kirafiki, michuano ya Kagame na Ngao ya Jamii, imefunga mabao 20.
Safu ya ushambuliaji ya timu hiyo inaongozwa na Kipre Tchetche, John Bocco, Leonel Saint-Preux, Didier Kavumbagu.
Licha  ya Azam kuonekana iko kamili kwa kuzifumania nyavu, ukuta wake imeonekana kulegalega kwani katika michezo 12, safu ya ulinzi imeruhusu mabao 11.
Safu ya ulinzi inaongozwa na Mwadini Ally, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni , David Mwantika/Said Morad na  Aggrey Morris.
Timu nyingine inayopewa nafasi ya kutisha ni Simba ingawa imeonekana haisomeki kwani bado inayumba katika safu yake ya ulinzi baada ya kumuondoa  Donald Mosoti, hivyo kubaki na beki mzoefu, Joseph Owino ambaye atasaidia na chipukizi Hassan Isihaka na Joram Mgeveke.
Simba imeonekana kuwa na safu bora ya ushambuliaji katika mechi sita za kirafiki ilizocheza, imefunga mabao 12 na imefungwa matatu, safu ya ushambuliaji inayoongozwa na Ammis Tambwe, Emmanuel Okwi, Elius Maguri, Paul Kiongera, Ramadhan Singano na Haruna Chanongo.

No comments:

Post a Comment

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia mkito.com!

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia  mkito.com !  Bila shaka utakuwa umeusikia huu wimbo kw...