welcome

Your welcome to Leyla Nyenzi Blog, Dodoma-Tanzania, for the only latest Audio's,Video's,Photo's, Events and Advertisement.

Thursday, 27 November 2014

Arsenal yafuzu,Liverpool yatoka sare

Yaya Sanogo afunga bao lake la kwanza katika mechi dhidi ya Borussia Dortmund .Arsenal ilishinda kwa mabao 2-0
Yaya Sanogo aliifungia Arsenal bao lake la kwanza walipoizaba kilabu ya Borusia Dortmund na kuhakikisha wamefuzu katika hatua ya muondoano wa michuano ya kombe la kilabu bingwa barani Ulaya.
Mshambuliaji huyo wa miaka 21 alifunga bao hilo baada ya kushiriki katika mechi 19 bila bao lolote alipomaliza pasi kati yake na Santi carzola mda mchache tu baada ya mechi kuanza.
Alexis Sanchez alifanya mambo kuwa 2-0 baada ya mda wa mapumziko alipopachika bao lililowaacha wengi vinywa wazi.
Vilevile mlinda Lango wa Dortmung aliokoa shambulizi la Sanchez mda mchache baadaye, huku shambulizi jengine la kiungo wa kati wa Arsenal Alex Oxlaide Chamberlain likigonga chuma cha goli.
Arsenal kwa mara ya kwanza walionyesha mchezo uliokomaa huku mabeki wake waliolaumiwa kwa msururu wa matokeo mabaya wakijitahidi vilivyo.
Wachezaji hao waliwazuia washambuliaji wa Dortmund akiwemo Pierre Aubemayang ambaye alikuwa moto wa kuotoa mbali wakati timu hizo mbili zilipokutana kwa mechi yao ya kwanza nchini Ujerumani.

Wakati huohuo Mkufunzi wa timu ya Liverpool Brendan Rodgers amesema kuwa amefurahishwa na hatua ya timu yake kuchukua udhibiti wa hatma yao hadi mechi ya mwisho katika michuano ya kufuzu kwa raundi za muondoano wa ligi ya kilabu bingwa Ulaya.
Timu hiyo ilifungwa bao la pili katika mda wa majeruhi na kilabu ya Bulgaria Ludogorets na kutoka sare ya 2-2 lakini bado watafuzu katika michuano ya raundi ya maondoano iwapo wataifunga timu ya Bacel mwezi Ujao.
Katika matokeo mengine:
Atl Madrid 4 - 0 Olympiakos
Malmö FF 0 - 2 Juventus
FC Basel 0 - 1 Real Madrid
Zenit St P 1 - 0 Benfica
Bayer Levkn 0 - 1 Monaco
Anderlecht 2 - 0 Galatasaray

No comments:

Post a Comment

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia mkito.com!

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia  mkito.com !  Bila shaka utakuwa umeusikia huu wimbo kw...