welcome

Your welcome to Leyla Nyenzi Blog, Dodoma-Tanzania, for the only latest Audio's,Video's,Photo's, Events and Advertisement.

Wednesday, 3 December 2014

HIZI NDIZO NCHI ZINAZOONGOZA KWA UFISADI AFIKA MASHARIKI:Burundi,UG na Kenya

Shrika la Ti limeyaorodhesha mataifa ya Uganda,kenya na Burundi kama yalio na ufisadi mkubwa

Baadhi ya fedha zinazotumika na mataifa ya Afrika mashariki.
Ufisadi nchini Kenya bado uko katika kiwango cha juu licha ya juhudi kukabiliana na swala hilo nyeti.
Kulingana na ripoti ya shirika la Tranparency International ya mwaka 2013,kenya imerodheshwa ya 136 kati ya mataifa 177 ikiwa na alama 27 katika kipimo cha 0-100.
Sufuri ina maanisha kwamba ufisadi umekithiri huku na 100 ikionyesha kwamba taifa hilo halina ufisadi.
Hatahivyo ni taifa la Burundi lenye ufisadi mkubwa miongoni mwa mataifa ya Afrika mashariki likifuatiwa na Uganda na baadaye Kenya kulingana na utafiti huo.
Kulingana na mkurugenzi wa shirika hilo nchini Kenya Samuel Kimeu,Kenya haijabadilika katika nafasi yake tangu mwaka 2012.
Amesema kuwa taasisi za umma zinahitajika kuwa wazi kuhusu maamuzi yao .
Katika afrika mashariki ,ni taifa la Rwanda Pekee ambalo limeonyesha juhudi za kukabiliana na ufisadi.
Rwanda imeorodheshwa ya 49 ikiwa na alama 54,Ushelisheli iko katika nafasi ya 47 ikiwa na alama 54 na Mauritius ikiwa katika nafasi ya 52 ikiwa na alama 52 ikitamatisha mataifa matano bora barani Afrika.
Botswana imesalia kuwa taifa ambalo halina ufisadi barani Afrika likiwa katika nafasi ya 30 na alama 64 likifuatiwa na Cape Verde ilio katika nafasi ya 41 na alama 58.Baadhi ya mataifa yalio na ufisadi duniani ni Somali,Sudan,Sudan Kusini Libya na Guinea Bissau.
chanzo:bbc swahili

No comments:

Post a Comment

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia mkito.com!

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia  mkito.com !  Bila shaka utakuwa umeusikia huu wimbo kw...