welcome

Your welcome to Leyla Nyenzi Blog, Dodoma-Tanzania, for the only latest Audio's,Video's,Photo's, Events and Advertisement.

Sunday, 30 November 2014

FIFA:Madai mapya ya ufisadi yazuka

Rais wa FIFA Sepp Blatter akiikabidhi Qatar mkataba wa kuandaa kombe la dunia la mwaka 2022.
Madai zaidi yameibuka kuhusu ufisadi uliofanyika wakati wa shughuli ya kuwatafuta waandalizi wa kombe la dunia la mwaka 2018 na 2022.
Rais wa FIFA Sepp Blatter akimkabidhi rais wa Urusi Vladmir Putin Haki za kuandaa dimba la dunia la mwaka 2018
Nafasi hizo zilichukuliwa na Urusi pamoja na Qatar. Gazeti la Sunday Times nchini Uingereza limesema kuwa rais wa Urusi Vladimir Putin alihusika pakubwa wakati nchi yake ilipokuwa ikitafuta nafasi hiyo na hata alimuomba rais wa FIFA Sepp Blattter kuisaidia kupata kura.
Pia kuna madai kuwa nchi ya Qatar ilitumia ushawishi wake katika sekta ya gesi kupata kura kupitia kandarasi za kibiashara.
Urusi na Qatar zimekana kuhusika kwenye vitendo hivyo na ziliondolewa lawama na shirikisho la soka duniani FIFA hivi majuzi.

No comments:

Post a Comment

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia mkito.com!

Kuwa wa kwanza kupata ladha kutoka kwa wakali wa huu muziki Afrika Kusini kupitia  mkito.com !  Bila shaka utakuwa umeusikia huu wimbo kw...